1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Jammeh aapa kutoondoka madarakani

Sudi Mnette
23 Desemba 2016

Rais Yahya Jammeh wa Gambia akaidi kuachia madaraka, licha kushindwa uchaguzi wa Desemba Mosi na kutakiwa na Jumuiya ya Uchumi ya Afrika Magharibi, ECOWAS, kuondoka au akabiliwe na hatua za kijeshi.

https://p.dw.com/p/2Uiwa
Gambia Präsident Yahya Jammeh & Nigerias Präsident Muhammadu Buhari
Rais wa Gambia Yahaya Jammeh akimpkea rais Muhammadu Buhari wa NigeriaPicha: Reuters

Msimamo wa Jammeh umezusha wasiwasi  kimataifa juu ya hali ya baadaye ya  taifa  hilo  dogo la Afrika magharibi, wakati Umoja  wa  Afrika ukijiunga na viongozi wa Afrika kumtaka ajiuzulu. 

Jammeh  alisema  katika  hotuba  ndefu katika televisheni, kwamba  haki  zake  haziwezi  kukiukwa  na kukandamizwa na hatasalimu amri ya ECOWAS.

Gambia inakabiliwa na mkwamo wa muda mrefu wa kisiasa baada ya kiongozi huyo wa muda mrefu kusema  atasubiri  hadi  uamuzi  wa mahakama  utakapopatikana  Januari kabla ya  kukabidhi  madaraka. 

Jammeh, ambaye amekuwa madarakani kwa muda wa miaka 22, aliwashangaza  wadadisi  kwa  awali  kukubali kushindwa  katika  uchaguzi  wa  Desemba Mosi  dhidi  ya mpinzani  wake  Adama  Barrow, lakini  kubadilika  wiki moja  baadaye,  akikataa  matokeo  na  kuwasilisha pingamizi  mahakamani.