1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Je, Dlamini-Zuma ataweza kuiongoza Afrika kusimama imara?

23 Julai 2012

Kwa mara ya mwanzo Umoja wa Afrika umemchagua kiongozi mwanamke kuuongoza Umoja huo unaoyakusanya moja ya mataifa masikini kabisa duniani, huku dunia ikikabiliwa na changamoto kadhaa za kiuchumi na kisiasa.

https://p.dw.com/p/15dIk
Mkuu mpya wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Nkosazana Dlamini-Zuma.
Mkuu mpya wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Nkosazana Dlamini-Zuma.Picha: Reuters

Suali linaoulizwa na wengi ni ikiwa kuchaguliwa huku kwa mwanamke kuliongoza bara la Afrika kuna maana yoyote ile katika mabadiliko ya taswira ya uongozi kwenye vichwa vya Waafrika, wanaoaminika kumpa nafasi zaidi mwanamme katika utawala? Je, Afrika inaongoza njia kwa masuala ya usawa wa kijinsia? Na kubwa kuliko yote, je Dlamini-Zuma atafanya kipi kipya ambacho mtangulizi wake, Jean Ping wa Gambia, kilimshinda?

Othman Miraji anaongoza mjadala mbele ya kipindi cha Maoni kutoka Idhaa ya Kiswahili ya DW. Kusikiliza mjalada huo, tafadhali bonyeza alama ya spika za masikinioni hapo chini.

Mwendeshaji: Othman Miraji

Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman