1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

JERUSALEM: Mashambulizi ya Israel yaendelea Ukanda wa Gaza

25 Mei 2007
https://p.dw.com/p/CByV

Ndege za kivita za Israel zimeendelea kushambulia vituo vya Hamas katika Ukanda wa Gaza.Kwa mujibu wa ripoti ya vyombo vya habari,Wapalestina 4 walijeruhiwa katika mashambulizi hayo.Kwa upande mwingine,wanamgambo wa Kipalestina walivurumisha makombora katika ardhi ya Israel.Ripoti ya jeshi la Israel imesema,makombora hayo yaliangukia kaskazini mwa jangwa la Negev na hakuna aliejeruhiwa.Siku ya Alkhamisi,Rais Mahmoud Abbas wa Wapalestina alitoa wito wa kusitisha mashambulizi ya roketi kutoka Ukanda wa Gaza na kukubaliana na Israel kuweka chini silaha.