1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Jumuia ya SADC yakutana kesho

Oumilkher Hamidou29 Machi 2009

SADC yafikiria vikwazo dhidi ya Madagascar

https://p.dw.com/p/HMI1

Mbabane:

Viongozi wa jumuia ya maendeleo kusini mwa Afrika-SADC wanakutana kesho kwa mkutano wa dharura kuzungumzia uwezekano wa kuwekewa vikwazo viongozi wa kipindi cha mpito kisiwani Madagascar na rais wao Andry Rajoelina."Viongozi wa SADC watatathmini njia za kurejesha demokrasia,na taifa linaloheshimu sheria na katiba kisiwani Madagascar" imesema serikali ya Afrika kusini-Mwenyekiti wa sasa wa jumuia hiyo ya kimkoa."Viongozi wa mataifa yote wanachama wameahidi watahudhuria mkutano huo"imesema kwa upande wake wizara ya mambo ya nchi za nje ya Swazilanz.Haikutajwa lakini viongozi gani wa Madagascar wamealikwa mkutano huo.SADC inapinga kuutambua utawala mpya unaoongozwa na Andry Rajoelina kisiwani Madagascar.