1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KABUL: Shambulizi la NATO limeua hadi watu 45

22 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBpT

Shambulio la vikosi vya anga vya NATO,kusini mwa Afghanistan,limeua hadi watu 45.Ripoti za vyombo vya habari zinasema,si chini ya raia 25 ni miongoni mwa wale waliouawa katika shambulizi lililofanywa wakati wa usiku.Inaaminiwa kuwa wengine waliouawa,walikuwa wapiganaji wa Taliban.