1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KABUL: Washukiwa kuhojiwa Afghanistan

9 Oktoba 2006
https://p.dw.com/p/CD4W

Maofisa wa usalama nchini Afghanistan wanapanga kuwahoji washukiwa sita kuhusiana na mauaji ya waandishi wawili wa habari raia wa Ujerumani.

Karen Fischer na Christian Struwe, waliokuwa wakifanya kazi na shirika la habari la Deutsche Welle, walipigwa risasi juzi Jumamosi katika hema lao mkoani Beghlan, yapata kilomita 120 kaskazini mwa mji mkuu Kabul.

Msemaji wa Taliban amesema kundi hilo halikuhusika na mauaji hayo.