Kamishna mkuu wa shirika la wakimbizi la Umoja wa Mataifa akamilisha ziara yake Tanzania
16 Aprili 2010Matangazo
Kamishna mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi-UNHCR, Antonio Gutteres, amemaliza ziara yake nchini Tanzania huku akishuhudia zoezi la Tanzania kuwapa uraia zaidi ya wakimbizi laki moja na elfu sitini kutoka nchini Burundi ambao wamekuwa wakiishi Tanzania tangu mwaka 1972.
Mwandishi wetu Christopher Buke aliyefuatana na kamishna huyo ametutumia taarifa ifuatayo.
Mtayarishaji: Christopher Buke
Mpitiaji: Grace Patricia Kabogo
Mhariri: Josephat Charo