1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KAMPALA:Jeshi la Uganda ladhibiti usalama mpakani na DRC

23 Agosti 2007
https://p.dw.com/p/CBWg

Msemaji wa kikosi cha jeshi katika eneo la kusini magharibi mwa Uganda Tabaro Kiconco amesema kwamba kikosi chake kinadhibiti hali ya usalama katika eneo la mpaka wake na nchi jirani ya Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Kongo kutokana na hali mbaya ya usalama iliyosababisha takriban raia elfu kumi wa nchi hiyo jirani kutoroka siku ya jumanne na kuvuka mpaka kuingia nchini Uganda.

Shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia wakimbizi hata hivyo limesema wakimbizi 8,500 walirejea nchini mwao Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Kongo siku ya pili yake huku wakimbizi 1,500 wanawake na watoto wakiwa bado wameslaia nchini Uganda.