KARACHI: Mvua kubwa zimesababisha vifo
25 Juni 2007Matangazo
Takriban watu 220 wameuwawa katika mji wa Karachi nchini Pakistan kufuatia mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa.
Mvua hizo pia zimesababisha ukosefu mkubwa wa umeme.
Raia wenye hasira wamefanya vurugu kwa kuchoma matairi na kuyarushia mawe magari yanayopita barabarani.
Mtu mmoja ameuwawa katika vurugu hizo.
Hali mbaya ya hewa imeikumba Pakistan na nchi jirani yake ya India.
Wafanyakazi wa kutoa misaada waling’ang’ana mwishoni mwa wiki kusambaza misaada ya chakula kwa takriban watu laki mbili walioathirika kutokana na mafuriko katika jimbo la Andhra Pradesh kusini mwa India.