1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kenya yaangamiza bunduki 5,000

Sylvia Mwehozi
16 Novemba 2016

Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto, anasema zaidi ya bunduki 5,200 zimeteketezwa kwenye taifa hilo la Afrika Mashariki katika jitihada za kuzuia mzunguko wa silaha kuyafikia makundi ya kihalifu.

https://p.dw.com/p/2SlhG
Irak Kuwait Waffenschmuggel
Picha: Getty Images/AFP/N. Hashem

Ruto aliandika katika ukurasa wake wa Twitter kwamba serikali imeteketeza bunduki hizo hadharani ili kutuma ujumbe kwa wale wanaofanya biashara haramu ya silaha. 

Makamu huyo wa rais amesema silaha ndogo ndogo zinaleta kitisho kwa amani na utulivu wa Kenya kwa sababu zimekuwa ni rahisi kupatikana kwa bei nafuu na ni nyepesi kuzificha. 

Silaha hizo zilizokamatwa kutoka kwa wahalifu au kusalimishwa kwa hiari ziliharibiwa mjini Ngong, kusini magharibi mwa mji mkuu, Nairobi.

Ruto amewataka wale wote wanaomiliki silaha kinyume na sheria kuzisalimisha kwa jeshi la polisi.