1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kerry kujiunga na mazungumzo kuhusu Iran

23 Novemba 2013

Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Marekani John Kerry atajiunga na mazungumzo kuhusu mpango wenye utata wa kinuklia wa Iran mjini Geneva leo Jumamosi(23.11.2013).

https://p.dw.com/p/1AMoQ
U.S. Secretary of State John Kerry steps aboard his aircraft in Geneva, November 10, 2013. REUTERS/Jason Reed (SWITZERLAND - Tags: POLITICS)
Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani John KerryPicha: Reuters

Iran na mataifa sita yenye nguvu duniani zinaonekana kuwa katika ukingo wa kupata mafanikio katika mkwamo uliokuwapo kwa muongo mmoja sasa katika mzozo huo.

Mawaziri wa mambo ya kigeni wa China, Ufaransa , Uingereza na Ujerumani , Wang Yi, Laurent Fabius, William Hague na Guido westerwelle, wanatarajiwa kushiriki katika majadiliano makali kuhusiana na makubaliano ambayo Iran itazuwia shughuli zake za kinuklia ili kuweza kupata unafuu wa vikwazo vya kiuchumi.

Germany's Foreign Minister Guido Westerwelle gestures as he leaves the Intercontinental hotel on the third day of closed-door nuclear talks with Iran in Geneva November 9, 2013. REUTERS/Denis Balibouse (SWITZERLAND - Tags: POLITICS ENERGY)
Waziri Guido WesterwellePicha: Reuters

Tangazo hilo limekuja baada ya wanadiplomasia katika mji huo wa Uswisi kusema kuwa masuala muhimu katika mazungumzo hayo, ambayo yalianza siku ya Jumatano huenda yametatuliwa.

Maafikiano yakaribia

Mwanadiplomasia mwandamizi kutoka bara la Ulaya amewaambia waandishi habari mapema kuwa mawaziri wa mambo ya kigeni wa mataifa sita watakuja mjini Geneva iwapo tu kutakuwa na makubaliano ya kutiwa saini. "tumepiga hatua, ikiwa ni pamoja na masuala ya msingi," amesema mwanadiplomasia huyo.

Waziri wa mambo ya kigeni wa Urusi Sergei Lavrov amewasili mjini Geneva siku ya Ijumaa jioni na amekutana na waziri wa mambo ya kigeni wa Iran Mohammad Javad Zarif na mkuu wa sera za mambo ya kigeni wa Umoja wa Ulaya Catherine Ashton, amesema msemaji wa Urusi.

Russian Foreign Minister Sergei Lavrov gestures during a news conference following his meeting with his Egyptian counterpart Nabil Fahmy in Moscow September 16, 2013. Lavrov said on Monday it may be time to consider efforts to force foes of Syrian President Bashar al-Assad to attend an international peace conference instead of just urging them to do so. REUTERS/Sergei Karpukhin (RUSSIA - Tags: POLITICS HEADSHOT)
Sergei Lavrov wa UrusiPicha: Reuters

Kerry anakwenda mjini Geneva " akiwa na lengo la kuendeleza hatua ya kupunguza tofauti na kusogea karibu na makubaliano," msemaji wa wizara ya mambo ya kigeni ya Marekani Jen Psaki amesema. Uamuzi ulichukuliwa baada ya kushauriana na Ashton , ambaye ni mratibu wa mazungumzo hayo na Iran kwa niaba ya mataifa ya Marekani , Urusi , China , Ufaransa, Uingereza na Ujerumani, amesema Psaki.

Mkwamo huenda umemalizika

Baadaye naibu msemaji wa wizara ya mambo ya kigeni ya Marekani Marie Harf amesema kuwa Kerry ameamua kwenda mjini Geneva "kutokana na hatua za maendeleo zilizofikiwa" na akiwa na "matumaini kwamba makubaliano yatafikiwa".

Likielezea matumaini kwamba makubalino yako karibu, shirika la habari la China Xinhua limemnukuu msemaji wa mambo ya kigeni wa nchi hiyo akisema kuwa mazungumzo hayo " yamefikia hatua za mwisho". Waziri wa mambo ya kigeni wa nchi hiyo ameondoka mjini Beijing kwenda Geneva mapema leo Jumamosi (23.11.2013).

Chinese Ambassador to Japan Wang Yi speaks during a news conference at the Foreign Correspondents' Club of Japan in Tokyo Thursday, Nov. 24, 2005. Wang said that resolving the dispute over a controversial Tokyo war shrine is "the urgent" issue facing Japan and China, and urged the Japanese government to call off visits by the prime minister. (AP Photo/Koji Sasahara)
Wang Yi wa ChinaPicha: AP

Wanadiplomasia wamesema kuwa maridhiano kuhusiana na msisitizo wa Iran kwamba "haki yake" ya kurutubisha madini ya urani itambulike kimataifa imependekezwa, huenda ikafungua njia ya kupatikana kwa maendeleo katika mkwamo uliopo.

Mwandishi: Sekione Kitojo / rtre

Mhariri: Bruce Amani