1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kesi wanaoshukiwa kutaka kuipindua serikali Ujerumani yaanza

29 Aprili 2024

Kesi ya kwanza kati ya tatu inayohusishwa na njama ya mapinduzi ya mrengo wa kulia inaanza nchini Ujerumani leo Jumatatu, huku washtakiwa wakituhumiwa kujiandaa kufanya uhaini mkubwa na kuhusishwa na kundi la kigaidi

https://p.dw.com/p/4fI8G
Msako wa kuwakamata watuhumiwa hao uliendeshwa na polisi mnamo Disemba 7, 2022.
Msako wa kuwakamata watuhumiwa hao uliendeshwa na polisi mnamo Disemba 7, 2022.Picha: Fricke/NEWS5/AFP

Washukiwa wote kwenye kesi hiyo ni sehemu ya vuguvugu la siasa kali  linajiita  "Reichsbürger" wakidaiwa kupanga njama ya kupindua serikali ya Ujerumani.

Kundi hilo linaupinga mfumo wa serikali ya Ujerumani uliowekwa baada ya vita, likidai uliwekwa na kudhibitiwa na Madola washirika yenye nguvu yaliyoshinda Vita vya Pili vya Dunia.

Polisi walifichua njama hiyo  katika msururu wa matukio ya msako uliofanywa  nchi nzima mnamo Desemba 7, 2022.  Takriban watu 25 walikamatwa na sasa wako kizuizini wakisubiri kesi zao.  Zaidi ya bunduki 380 zilipatikana, pamoja na karibu silaha 150,000.

Washtakiwa hao tisa wanawakilishwa na mawakili 22, huku mashahidi zaidi ya 300 wakitajwa, wakiwemo askari polisi 270.