1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KHARTOUM : 30 wauwawa katika shambulio Dafur

11 Desemba 2006
https://p.dw.com/p/CCkM

Katika jimbo la vurugu nchini Sudan la Dafur takriban raia 30 wameuwawa na watu waliokuwa na silaha wakiwa wamepanda farasi ambao walilishambulia gari lililokuwa limebeba misaada ya madawa na ile ya faraja.

Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema baadhi ya wahanga walipigwa risasi wakati wengine walitiwa moto wakati wakiwa hai. Wanamgambo wa Kiarabu wanaojulikana kama Janjaweed wanatuhumiwa kuhusika na shambulio hilo.Hali inayozidi kuwa mbaya huko Dafur imeulazimisha Umoja wa Mataifa na mashirika ya misaada kuwaondowa wafanyakazi wao wengi.

Serikali ya Sudan mara kadhaa imelikataa azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lenye kutaka kuwekwa kwa wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa huko Dafur kwa kusema kwamba kikosi hicho kitakuwa na sawa na kile cha ukoloni.