Binti wa darasa la tatu kutoka familia ya wafugaji nchini Tanzania, amekatiza masomo yake baada ya kupewa ujauzito na kuwaacha katika majonzi wazazi waliokuwa wamewekea matumaini yao kwake. Hawa Bihoga anaangalia masahibu yanayomkuta binti huyo na wazazi wake, hasa kwa kuzingatia ukweli kwamba hawezi tena kuruhusiwa shuleni kutokana na amri ya Rais John Magufuli. Ni makala ya Mbiu ya Mnyonge.