1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kim Jong Il afariki dunia

Mohammed Khelef19 Desemba 2011

Televisheni ya serikali ya Korea ya Kaskazini imetangaza kuwa kiongozi wa nchi hiyo, Kim Jong Il, amefariki dunia akiwa na umri wa mika 69. Kabla ya kifo chake, inaaminika kuwa Kim alikuwa akiugua sukari na moyo

https://p.dw.com/p/13VHQ
Kim Jong Il (kulia) na mtoto wake Kim Jong Un katika picha ya mwaka 2010.
Kim Jong Il (kulia) na mtoto wake Kim Jong Un katika picha ya mwaka 2010.Picha: picture-alliance/dpa

Kim alikuwa pia akiugua maradhi ya kiharusi tangu mwaka 2008, lakini aliwahi kuonekana katika picha akiwa kwenye ziara za karibuni nchini China na Urusi na nyengine ndani ya nchi yake, ambazo zilikuwa zikitolewa na vyombo vya habari vya serikali. Kiongozi huyo wa Kimomunsti aliyekuwa akijuilikana kwa jina la “Kiongozi Mpenzi” anakumbukwa kwa kupenda kwake sigara, konyagi na vyakula vya kifahari.