1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kinshasa. Bemba akataa matokeo ya uchaguzi, aweka pingamizi.

19 Novemba 2006
https://p.dw.com/p/CCrV

Jean-Pierre Bemba mgombea aliyeshindwa katika duru ya pili ya uchaguzi wa rais katika jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo , jana alitoa pingamizi rasmi dhidi ya matokeo ya uchaguzi huo , ambao umempatia ushindi rais wa sasa Joseph Kabila.

Kuna idadi kadha ya matukio ya uendeaji kinyume uchaguzi huu na ambayo yamesababisha udanganyifu katika matokeo hayo , ambayo yameatangazwa na tume huru ya uchaguzi.

Kwa mujibu wa ahadi zilizotolewa na mgombea Jean-Pierre Bemba , tumekuja katika mahakama kuu kupinga dhidi ya mapungufu haya , amesema Delly Sessanga, msemaji wa muungano wa umoja wa kitaifa unaoongozwa na Bemba.

Alikuwa Sessanga ambaye amewasilisha pingamizi hiyo dhidi ya matokeo ya uchaguzi kwa niaba ya Bemba , kiongozi wa zamani wa waasi ambae hivi sasa ni mmoja kati ya makamu watano wa rais katika jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo na mmoja kati ya watu tajiri sana.