1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KINSHASA: Machafuklo yazuka nchini Kongo

27 Oktoba 2006
https://p.dw.com/p/CCyo

Machafuko yameripotiwa nchini Jamhuri ya Kodemokrasi ya Kongo huku duru ya pili ya uchaguzi wa rais ikiaribia kufanyika mwishoni mwa juma.

Imeripotiwa watu wasiopungua wanne wameuwawa kwenye mapigano kati ya wafuasi wa rais Joseph Kabila na mpinzani wake mkuu Jean Pierre Bemba katika mji wa Gbadolite, kaskazini magharibi mwa Kongo.