1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KINSHASA;Baraza jipya la mawaziri nchini J.KKongo

6 Februari 2007
https://p.dw.com/p/CCUh

Baada ya kuchelewa kwa wiki kadhaa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo imepata baraza jipya la mawaziri.

Waziri Mkuu bwana Antoine Gizenga aliteuliwa na rais Joseph Kabila mapema mwezi desema na mawaziri wengine wametangazwa kwa njia ya televisheni.

Waziri Mkuu Gizenga na mawaziri wake wanakabiliwa na changamoto kubwa ya kuijenga upya nchi yao baada ya vita vya muda mrefu vilivyozihusisha nchi jirani vilevile. Watu wapatao milioni nne walikufa kutokana na vita hivyo kati ya mwaka 1998 na 2003.