KISMAYU: Maelfu ya wasomali waukimbia uwanja wa vita
31 Desemba 2006Matangazo
Maelfu ya wasomali wameanza kuukimbia uwanja wa vita huku wanajeshi wa Ethiopia waliojihami na silaha nzito wakisaidiwa na ndege za kivita wakiikaribia ngome iliyosalia ya wanamgambo wa mahakama za kiislamu mjini Kismayu.
Wasomali takriban 2,000 wamebeba walichoweza na kuukimbia mji wa kusini wa Jilib ambako wanamgambo wasiopungua 3,000 wa mahakama za kiislamu wamejificha kati ya mpaka wa Kenya na bahari ya Hindi wakijiandaa kupigana kufa kupona na majeshi ya Ethiopia.
Mabomu ya kutegwa ardhini yaliyozikwa kwenye njia inayoelekea Kismayu yanawachelewesha wanajeshi wa serikali ya mpito ya Somalia na majeshi ya Ethiopia kuufikia mji huo.