1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kombe la BDF Bayern yaingia kwa kishindo robofainali

23 Desemba 2010

Bayern Munich, Duisburg, Alemannia Aachen na Energie Cottbus zimefanikiwa kuingia robo fainali ya kombe la shirikisho la soka la Ujerumani BDF baada ya kushinda hapo jana.

https://p.dw.com/p/zoe9
Franck Ribery(kushoto) na Mario Gomez wakishangilia moja ya mabao waliyoifungia Bayern dhidi ya VfB StuttgartPicha: AP

Bayern ambao ni mabingwa watetezi wa kombe hilo la DFB ilivurumisha VfB Stuttgart, kwa mabao 6-3, ambapo Miroslav Klose alipachika mabao 2 kati ya hayo.

Bayern sasa katika robofainali itapambana na Alemannia Aachen ambayo iliipiga kumbo Eintracht Frankfurt katika mechi iliyoamuliwa kwa changamoto ya penalti, baada ya kuwa sare ya bao 1-1 hadi mpambano ulipoisha.Aachen walitumbukiza penalti nne wakati Frankfurt walipata mbili.

Nayo timu ya daraja la pili Energie Cottbus, iliwaaibisha VfL Wolfsburg inayoshiriki katika Bundesliga kwa kuichapa mabao 3-1 na kufuzu kwa robofainali.Cottbus sasa itapambana na Hoffenheim katika robofainali.

Timu nyingine ya Bundesliga FC Cologne iliadhiriwa na timu ya daraja la pili Duisburg kwa kuchapwa mabao 2-1 na kusukumizwa nje ya michuano hiyo.

Mwandishi:Aboubakary Liongo