1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Komorowski ashinda uchaguzi wa rais Poland

5 Julai 2010

Bronislaw Komorowski, ameshinda duru ya pili ya uchaguzi wa rais uliofanywa siku ya Jumapili nchini Poland.

https://p.dw.com/p/OAdx
Parliament Speaker, acting president Bronislaw Komorowski with wife Anna enter a voting station in Mackowa Ruda, northeast Polan, Sunday, July 4, 2010. Poles are choosing their new president in the runoff presidential elections, between Komorowski and Jaroslaw Kaczynski, twin brother of the late President Lech Kaczynski who was killed in a plane crash.(AP Photo/Alik Keplicz)
Bronislaw Komorowski na mkewe Anna.Picha: AP

Kwa mujibu wa televisheni ya taifa TVP, Komorowski amejikingia asilimia 53 ya kura zilizopigwa wakati mpinzani wake, Jaroslaw Kaczynski amepata asilimia 47.

Kaczynski ni kiongozi wa chama kikuu cha upinzani kinachofuata sera za mrengo wa kulia, "Law and Justice" na ni ndugu pacha wa rais Lech Kaczynski alieuawa katika ajali ya ndege mwezi wa Aprili.Uchaguzi wa rais umeitishwa kufuatia kifo hicho.

Matokeo ya uchaguzi huo humaanisha kuwa Komorowski wa chama cha kiliberali cha "Civic Platform" na mshirika wake wa karibu, Waziri Mkuu Donald Tusk wataweza kuidhinisha marekebisho ya kifedha kabla ya uchaguzi wa bunge uliopangwa kufanywa mwakani.

ARCHIV - Der polnische Ministerpräsident Donald Tusk am 11.12.2007 im Bundeskanzleramt in Berlin. Der Weg nach Europa war für den polnischen Regierungschef Donald Tusk alles andere als bequem. Vor zwei Jahren noch gab es schwere Auseinandersetzungen um den Vertrag von Lissabon. Tusk setzte den Vertrag damals gegen seinen Widersacher Präsident Lech Kaczynski durch. Der Aachener Karlspreis erwähnt diesen Vertrags-Erfolg ausdrücklich. Tusk sei ein Patriot und großer Europäer, heißt es. Am 13. Mai erhält der Pole den renommiertesten Europa-Preis nach gerade einmal zweieinhalb Jahren Amtszeit. Bundeskanzlerin Merkel hält die Laudatio. Foto: Wolfgang Kumm dpa/lnw +++(c) dpa - Bildfunk+++
Waziri Mkuu wa Poland,Donald Tusk.Picha: picture alliance/dpa

Kwa mujibu wa Katiba ya Poland, wajibu wa rais sio kuliwakilisha taifa tu bali ana mamlaka yake hasa katika sera za nje na usalama. Jaroslaw Kaczynski amekubali kuwa ameshindwa na amempongeza mpinzani wake Komorowski.

Mwandishi:P.Martin/RTRE/DPA

Mhariri: Mwadzaya,Thelma