1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

LONDON ; Meli yaponea chupu chupu kugonga jukwaa la gesi

12 Januari 2007
https://p.dw.com/p/CCbZ

Meli ya mizigo katika Bahari iliochafuka ya kaskazini imeponea chupu chupu kugongana na majukwa mawili ya gesi baharini na tishio hilo lililazimisha wafanyakazi watelekeze mojawapo ya majukwaa hayo na kusitisha uzalishaji.

Tishali moja liko njiani kwenda kuivuta meli hiyo ufukweni inayoitwa Vindo na wafanyakazi wake tisa

Awali ilielezwa kwamba meli hiyo ya tani 3,000 iliopoteza nguvu za engine yake ilikuwa igongane na jukwaa hilo la gesi wakati ikielea kati ya Scotland na Norway.

Hali ya tahadhari ilitangazwa hapo jana usiku baada ya meli hiyo ilioandikishwa Antigua na Bermuda ikiwa na shehena ya tani 4,200 za mbolea ilipokuwa ikielea karibu na majukwaa hayo ya kuchimba gesi baharini.