LUXEMBOURG:Mawaziri washindwa kuafikiana
18 Juni 2007Matangazo
Mawaziri wa mambo ya nje wa nchi za Umoja wa Ulaya wamemaliza mazungumzo yao mjini Luxembourg bila ya kupiga hatua katika kuondosha vizingiti vinavyozuia mapatano juu ya mkataba mpya wa mageuzi.
Akizungumza baada ya mkutano huo waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani bwana Frank- Walter Steinmeier amesema kuwa hana uhakika iwapo suluhisho litapatikana kabla ya kufanyika mkutano mkuu wa viongozi wa Umoja huo alhamisi ijayo.