1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maandamano kuendelea Ukraine

1 Desemba 2013

Upinzani nchini Ukraine unamatumaini kuwa waandamanaji hadi alfukumi watajitokeza leo(01.12.2013)Jumapili na kutoa msukumo mpya kudai rais Viktor Yanukovich ajiuzulu kutokana na mzozo wa uhusiano na Umoja wa Ulaya.

https://p.dw.com/p/1AR9E
General view of Independence Square during a demonstration in support of EU integration, in Kiev November 29, 2013. Ukrainian President Viktor Yanukovich's decision to walk away from a deal that would have aligned his former Soviet republic more closely with the European Union sparked both anger and applause on the streets of Kiev on Friday. A sea of blue and gold, the colours of both the EU and Ukrainian flags, swept through the capital as people joined rival protests - one to celebrate closer ties with Russia, another to lament what they saw as a lost chance. REUTERS/Vasily Fedosenko (UKRAINE - Tags: POLITICS CIVIL UNREST CITYSCAPE)
Maandamano mjini KievPicha: Reuters

Vyama vikuu vitatu vya upinzani vimesema vinaanzisha , "kikosi cha taifa cha upinzani" baada ya polisi wa kuziwia ghasia kuwatawanya waandamanji kwa kutumia nguvu na kuwajeruhi watu kadha jana Jumamosi.

Mkutano huo wa waungaji mkono upinzani ulivunjwa na polisi waliotumia virungu ambao waliwashambulia kiasi ya waandamanaji 1,000 katika uwanja wa uhuru katika mji mkuu Kiev mapema jana Jumamosi asubuhi(30.11.2013).

People supporting EU integration hold a rally in front of the Mikhailovsky Zlatoverkhy Cathedral (St. Michael's Golden-Domed Cathedral) in Kiev November 30, 2013. Ukraine's political opposition on Saturday said it would call a country-wide general strike to force the resignation of President Viktor Yanukovich's government after police used batons and stun grenades to break up pro-Europe protests. REUTERS/Vasily Fedosenko (UKRAINE - Tags: POLITICS CIVIL UNREST)
Maandamano mjini KievPicha: Reuters

Kiasi ya watu 10,000 walikusanyika katikati ya mji wa Kiev usiku wa Ijumaa na kusema Yanukovich ajiuzulu baada ya rais huyo kukataa kutia saini makubaliano ya kisiasa na kibiashara pamoja na Umoja wa Ulaya.

Maandamano zaidi

Upinzani umetoa wito wa kufanyika maandamano mapya leo katikati ya mji wa Kiev baada ya polisi kuzingira uwanja huo wa uhuru kwa kuweka uzio wa chuma.

"Tunaweza na tunapaswa kuwaondoa viongozi hawa," bingwa wa dunia wa ngumi Vitali Klitschko , kiongozi wa chama cha UDAR amewaambia waungaji mkono upinzani wapatao 10,000 siku ya jumamosi, na kutangaza maandamano mapya.

Ukrainian heavyweight boxing superstar Vitali Klitschko gives a thumbs up as he and his wife Natalya (R) leave a polling station after casting their ballots, in Kiev on October 28, 2012, during national parliamentary elections. Ukraine voted today in legislative polls seen as a test of democracy under President Viktor Yanukovych with jailed opposition leader Yulia Tymoshenko forced to watch from the sidelines. AFP PHOTO / ALEXANDER NEMENOV (Photo credit should read ALEXANDER NEMENOV/AFP/Getty Images)
Vitali Klitschko kiongozi wa chama cha UDARPicha: Getty Images

"Tunapaswa kujitokeza na kuonesha kuwa hatutawaruhusu kutudhalilisha, tutasimama na kudai haki zetu," ameuambia mkusanyiko huo karibu wiki moja baada ya maandamano makubwa ya umma kuzuka nchini Ukraine kufuatia uamuzi wa maafisa kuachana na mpango wa kutia saini makubaliano na Umoja wa ulaya ambayo yangeiweka jamhuri hiyo ya zamani ya Umoja wa Kisovieti katika njia kuelekea kujiunga na Umoja wa Ulaya. Umoja wa Ulaya umeishutumu Urusi kwa kuipa mbinyo Ukraine, nchi ambayo inategemea kwa kiasi kikubwa gesi kutoka Urusi, na kujitoa kutoka katika makubaliano hayo.

Matumizi ya nguvu na vitisho

Jana Jumamosi , Lithuania ambayo inashikilia uongozi wa Umoja wa Ulaya kwa sasa imesema matumizi ya nguvu "hayavumiliki" na mkuu wa sera za mambo ya kigeni wa Umoja huo Catherine Ashton pamoja na kamishna wa upanuzi wa Umoja huo Stefan Fuele wametoa wito wa kufanyika uchunguzi.

European Union High Representative for Foreign and Security Policy Catherine Ashton speaks to journalists prior to a meeting of Ministers for Foreign Affairs in the Palace of the Grand Dukes of Lithuania in Vilnius on September 6, 2013. AFP PHOTO / TOMAS LUKSYS (Photo credit should read TOMAS LUKSYS/AFP/Getty Images)
Mkuu wa sera za mambo ya kigeni wa EU, Catherine AshtonPicha: TOMAS LUKSYS/AFP/Getty Images

"Matumizi ya nguvu na vitisho havina nafasi katika Ukraine ya leo," ameongeza msemaji wa wizara ya mambo ya kigeni wa Marekani, Jen Psaki

Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limetoa wito kwa maafisa nchini Ukraine kutimiza wajibu wao wa kulinda haki za binadamu.

Jana Jumamosi, Yanukovich alisema katika taarifa kuwa, "amefadhaishwa mno" na matumizi ya nguvu dhidi ya waandamanaji na ameapa kuwa waliohusika wataadhibiwa.

Mwandishi: Sekione Kitojo / afpe

Mhariri: Grace Patricia Kabogo