1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MADRID: Washukiwa ugaidi wakamatwa Uhispania

21 Septemba 2007
https://p.dw.com/p/CBO3

Raia 2 wa Pakistani wamekamatwa nchini Uhispania wakishukiwa kusaidia kifedha,vitendo vya ugaidi duniani.Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Ndani imesema,washukiwa hao walikamatwa katika uvamizi uliofanywa kwenye miji ya Madrid na Barcelona.Hatua hiyo ilichukuliwa kufuatia operesheni ya ushirikiano ya miaka mitatu,kati ya polisi ya Uhispania na Shirika la Upelelezi la Marekani,FBI.