Profesa Said Ahmed Mohammed Khamis anatambuliwa kama bingwa wa fasihi andishi ya Kiswahili, akiwa hadi sasa ameshachapisha zaidi ya kazi 40 ndani ya kipindi cha miaka 40 ya uandishi wake, zikiwemo riwaya, hadithi fupi fupi, tamthilia na ushairi. Katika mazungumzo haya na Mohammed Khelef anazungumzia maendeleo ya fasihi andishi kwenye ulimwengu wa Kiswahili.