1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mageuzi yaliyopendekezwa na Kagame yajadiliwa AU

Grace Kabogo
29 Januari 2018

Mageuzi kadhaa yaliyopendekezwa na Rais wa Rwanda, Paul Kagame ambaye pia ni mwenyekiti mpya wa Umoja wa Afrika kwa ajili ya kujitegemea kifedha kwa Umoja wa Afrika yamejadiliwa kwenye kikao cha 30 cha marais na viongozi wa serikali wa nchi wanachama wa umoja huo.

https://p.dw.com/p/2riI0

Lakini mageuzi hayo yatachukuwa muda kabla ya kufikia malengo yake ambayo ni kujitegemea kifedha kwa Umoja wa Afrika.

Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa wa Tanzania, Dokta Augustine Mahiga ambae ameongoza ujumbe wa nchi yake mjini Addis Ababa, Ethiopia ameelezea masuala muhimu yaliyojadiliwa kwenye kikao hicho ikiwemo ufumbuzi wa mizozo ya kikanda.

Kwenye mahojiano ya kipekee na mwandishi wetu Saleh Mwananamilongo, Balozi Mahiga ameanza kwanza kuelezea agenda ya mkutano huo.