1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mahakama ya uhalifu ya ICTR mjini Arusha,Tanzania, imewahamisha wafungwa tisa nchini Mali

12 Desemba 2008

Nchini Tanzania mahakama ya uhalifu kwa ajili ya Rwanda ICTR iliyoko mjini Arusha imewahamishia nchini Mali wafungwa tisa ili kutumikia vifungo vyao.

https://p.dw.com/p/GEhF
Mtaa mojawapo wa Arusha kwenye mahakama ya uhalifu ICTRPicha: dpa - Bildarchiv

Hatua hii ilifanyika kwa mara ya mwisho mwaka 2001.Kulingana na sheria ya 26 ya mahakama hiyo ya ICTR wafungwa hao kamwe hawawezi kutumikia vifungo vyao nchini Tanzania ila wanaweza kurejeshwa nchini mwao Rwanda au nchi nyengine iliyotia saini makubaliano na ICTR.Ifahamike kuwa hakuna hata mshtakiwa mmoja aliyewahi kutumikia kifungo chake Rwanda.

Kutoka Arusha Nicodemus Ikonko ana maelezo kamili.