Mahmud Abbas ziarani Riyadh
5 Januari 2008Matangazo
AMMAN:
Rais wa mamlaka ya Ndani wa Palestina Mahmud Abbas ameondoka Jordan kuelekea Riyadh,Saudi Arabia kushauriana na mfalme Abdullah juu ya hali ya mazungumzo ya amani ya Mashariki ya kati kabla rais George Bush hakuwasili huko wiki hii ijayo-duru za wapalestina zimearifu.
Rais Bush anaetarajiwa kuzuru Israel na ardhi za wapalestina amepinga mpango wa Israel wa kutanua ujenzi wa maskani za wayahudi katika ardhi za wapalestina.