1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Makampuni makubwa yahimizwa kupambana na biashara ya kuuza watu

mjahida5 Januari 2014

Washikadau wametoa wito kwa makampuni makubwa 15 nchini Marekani kuhakikisha kuwa kampuni zake zilizo nje ya nchi hazisaidi katika uvunjifu wa haki za binaadamu hasa kazi ngumu na bishara ya ngono.

https://p.dw.com/p/1AlOW
Menschenhandel, Moderne Sklaverei
Wanafunzi wakiromania wakitoa hamasa ya hatari ya biashara ya kuuza watu na ile ya ngono.Picha: AP

Katika kampeni itakayodumu mwezi mzima wa Januari, taasisi ya ICCR inayowakilisha mashirika ya washika dao 300 yanayoendesha mali ya takriban dola bilioni 100 inatoa umuhimu kwa sekta mbili kwa ujumla, ukarimu na kilimo cha chakula.

Sekta hizi zinajumuisha mahoteli, mashirika ya ndege, mikawaha, makampuni makubwa na makambuni yanayojishughulisha na kilimo yanayoonekana sana kuwa katika hatari ya kuvunjwa kwa haki za binaadamu.

Amol Mehra mkurugenzi wa shirika moja la kimataifa aliliambia shirika la habari la IPS kwamba katika kupambana na dhuluma kama biashara ya kuuza watu isiokubalika, kila mtu ana jukumu la kutekeleza na bishara inapaswa kuwa moja ya njia ya suluhu kuweka katika vitendo heshima ya haki za binaadamu na kuhakikisha wateja wake, maajenti, wafanyabiashara wenzao na hata wanaowauzia mali kuwa wanafuata mkondo mmoja.

ICCR sasa imetoa wito kwa makampuni makubwa 15 nchini Marekani kuchukua hatua katika suala hili. Makampuni haya ni kama ADM, ConAgra, Costco, Kroger, Target Walmart, mashirika ya ndege kama Delta, US Airways na Southwest pamoja na mahoteli kama Hyatt, Starwood, Choice na kadhalika.

Jemen afrikanische Migranten in Harad
Madhara ya biashara ya kuuza watu isiokubalikaPicha: DW/Alsoofi

Wanachama wa makundi haya hivi karibuni wametoa mikakati mipya itakayoongoza makampuni kuhakikisha kuwa wale wote walio na mkataba na kampuni hizo wanakubali kuafikia makubaliano ya kimataifa ikiwemo ule wa Umoja wa Mataifa juu ya Bishara na haki za binaadamu uliopitishwa mwaka wa 2011 yanayonuia kupiga vita aina yoyote ya biashara ya kuuza watu isiokubalika.

Makampuni pia yanatiliwa mkazo kuweka katika maandishi habari za mara kwa mara za namna wanavyokabiliana na suala hili na pia kuchambua hatari yake.

Njia zaidi za kupambana na kadhia hiyo zatolewa

Lauren Compere mwanachama wa ICCR amesema mahali ambapo makampuni yanakosa kuwepo katika viwango vinavyohitajiwa ni wakati panapokuja suala la ufichuzi, hasa katika sekta ya ukaribu kama vile hoteli, kufichua hatari ya kuwepo kwa hali ya dhuluma mbali mbali kunahitaji zaidi mfumo wa hadhi ya juu katika kuripoti.

Laureen amesema kwa sasa habari wanazozipata hazijachapishwa mahala popote au zinaosa ushahidi. Amesema kampuni nyengine zinaendelea vizuri kufichua visa vya uvunjifu wa haki za binaadamu na wala sio biashara ya kuuza watu isiokubalika.

Kulingana na shirika la kimataifa la wafanyakazi mwaka wa 2012 takriban watu milioni 14.2 wanafikiriwa kuhusishwa katika aina ya kazi za kulazimishwa huku wengine milioni 4.5 wamekuwa wakiingizwa katika biashara ya ngono.

Zwangsprostitution Prostitution Menschenhandel Deutschland
Miguu ya msichana aliyekatika biashara ya NgonoPicha: imago/EQ Images

“Mahoteli mikahawa na sekta nyengine za burudani, sana huonekna kukumbwa na biashara za ngono na tumeona kuwa iwapo watu wanaofaya biashara kama hizi watafungua mach yao basi hueda wakapata visa vingi vikienhdeea humo ndani,” Alisema Karen Stauss, mkurugenzi wa mpango wa kuachia watumwa.

Karen Stauss amesema kuwa katika sekta ya kilimo mambo ni tofauti kwa kuwa katika eneo hilo ndiko unakopata watu wanaopata mapato madogo sana na wanaotokea mashambani wakiwa na kiwango kidogo cha eliu na kutojua haki zao.

Sasa Stauss amesema hakuna njia yoyote ambapo wanaweza kusuluhisa sula la biashra ya kuuza watu isiokubalika hadi pale akapuni makubwa yatakapoungana pamoja na kujhusisha na kampeni ya kuupiga vita.

Mwandishi:Amina Abubakar/IPS

Mhariri:Sekione Kitojo