1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Makubaliano ya kuwarudisha watuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda 1994 yatiwa saini baina ya Rwanda na Kenya

30 Septemba 2009

<p>Nchi za Rwanda na Kenya zimetiliana saini makubaliano ya kuwarejesha nyumbani watuhumiwa wa mauaji ya halaiki yaliyotokea Rwanda mwaka 1994.

https://p.dw.com/p/JuzG
Makaburi ya wahanga wa mauaji ya halaiki 1994 nchini RwandaPicha: AP
Uamuzi huo umefikiwa wakati ambapo mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita kwa ajili ya Rwanda ICTR iliyoko mjini Arusha,Tanzania inajiandaa kuzikamilisha shughuli zake ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.Mataifa mengine ya Burundi,Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo bado yanaendelea na majadiliano ya kufikia mkataba wa aina hii.Mkataba wenyewe utaanza kutekelezwa baada ya siku sitini.Mwandishi wetu wa Kigali Daniel Gakuba alihudhuria shughuli hiyo na ameandaa taarifa ifuatayo:

Mwandishi: Daniel Gakuba

Mhariri: Othman Miraji