1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MALATYA UTURUKI:Watatu wachinjwa

19 Aprili 2007
https://p.dw.com/p/CC96

Watu watatu wameuawa katika shambulio kwenye nyumba ya uchapishaji kusini mashariki mwa Uturuki. Watu wengine wawaili walijeruhiwa katika shambulio

lililofanywa katika mji wa Malatya. Vyombo vya habari vimeripoti kuwa watu hao watatu wote walichinjwa. Mmoja wao anasemekana alikuwa mjerumani. Idara za usalama za Uturuki zimefahamisha kuwa nyumba hiyo inachapisha biblia na fasihi ya kikristo.