1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Uchumi

Mamia waandamana kupinga Wachina Kampala

19 Aprili 2017

Wafanyabiashara wa Kampala wamekusanyika katikati mwa mji kupinga kile wanachokitaja kuwa kunyanyaswa na raia wa China wanaofanya biashara za rejareja na kuuza bidhaa sawa na zao kwa bei ya chini.

https://p.dw.com/p/2bXBA
Soko jijini Kampala
Picha: DW/S. Schlindwein

J3.19.04.2017 Kampala Trader's Strike - MP3-Stereo

Mgomo huo umeungwa mkono na viongozi wa mji wakiwemo meya Erias Lukwago na mbunge wa eneo hilo Muhamad Nsereko ambaye amekamatwa na kuzuiliwa kwa muda na polisi kwa madai ya kuwachochea wafanyabiashara waafrika.