1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mamia wawakumbuka wasoshalisti wakijerumani Berlin

13 Januari 2008
https://p.dw.com/p/Cp2w

BERLIN:

Watu maelfu kadhaa wamekusanyika leo mjini Berlin kuwakumbuka washoshalisti wawili wa kijerumani-Rosa Luxemburg na Karl Liebkneicht, waliouliwa miaka 89 iliopita.

Miongoni mwa watu mashuhuri waliohudhuria ni mwenyekiti wa chama cha mrengo wa kushoto- Lothar Bisky na kiongozi wa kundi la wabunge wa chama hicho-Gregor Gysi.Luxemberg na Liebknecht waliuliwa na makamando wa mrengo wa kulia januari 15 mwaka wa 1919.