1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Magazetini.

Abdu Said Mtullya16 Septemba 2009

Wahariri wengi leo wanazungumzia mkasa wa kuuawa kwa mafanyabiashara kwenye kituo cha treni cha mjini Munic.

https://p.dw.com/p/Ji4A
Kituo cha treni cha Munic ambako mfanyabiashara alipigwa na vijana hadi alikufa.Picha: AP

Wahariri wengi leo  wanazungumzia mkasa uliotekea kwenye  kituo cha treni cha mjini Munic ambapo muungwana  mmoja  alipigwa na vijana wawili na kuuawa.Wahariri hao pia wanatoa maoni  yao juu  ya  mgogoro wa nyuklia wa Iran.
Mhariri  wa gazeti la Ostee Zeitung anamkumbuka  Patrick Swayze.

Jumamosi iliyopita vijana wawili walimpiga  na kumwuua mfanyabiashara mmoja  aliekuwa na umri  wa miaka 50  kwenye  kituo cha treni cha  mjini  Munic. Sababu  ni  kwamba mfanyabiashara  huyo  alijaribu  kuwalinda watoto  ili wasisumbuliwe na vijana hao wawili.

Juu  ya mauaji  hayo gazeti  la Dithmarscher Landeszeitung linasema, sasa  baada ya vijana  hao wawili kumpiga na kumwuua mfanyabiashara  huo, wanasiasa wanataka sheria  ziwe kali  zaidi.

Lakini mhariri wa  gazeti hilo anasema adhabu   kali hazitawasumbua  wauaji  hao.

Naye Mhariri wa gazeti la Emder Zeitung anakubaliana na hoja hiyo lakini anaeleza kuwa pana ushahidi unaoenyesha  kwamba sheria  kali peke yake hazitazuia  matendo  ya kutumia nguvu  miongoni  mwa vijana fulani.

Mhariri anasema polisi zaidi wanahitajika ili kuzuia vitendo vya ushari.

Katika maoni yake gazeti la Braunschweiger linasema vijana wauaji kama hao wawili lazima  wakomeshwe. Lakini wajibu huo usiwe  wa mwananchi mmoja peke yake.

Gazeti hilo  pia linatilia maanani ulazima  wa kuongeza idadi ya polisi ili kulinda usalama wa  wananchi.


Gazeti  la Münchner Merkur leo linazungumzia mvutano  baina ya Iran na nchi za  magharibi  kuhusiana  na mpango  wa nyuklia.Gazeti hilo linaeleza  kwamba hadi sasa hakuna dalili  zozote  juu  ya  kutatuliwa kwa mgogoro huo.

Mhariri huyo anasema  ikiwa Iran itaendelea na ukaidi nchi  za magharibi zitapaswa kujiuliza iwapo  zitakuwa tayari kuona  taifa lenye silaha  za nyuklia likizuka katika mashariki ya kati.?

Au nchi hizo zitachukua hatua kali?

Gazeti la Münchner Merkur linasema, ikiwa nchi za magharibi zitaamua kuchukua  hatua hizo  kali, Israel pia itapaswa ishiriki katika uamuzi ,kwa  sababu Israel ndiyo itakayotishiwa.   


Gazeti la Ostee Zeitung  linatoa salam za rambi rambi juu ya kifo cha mcheza senema maaruf  Patrick  Swayze  aliefariki  jana kutokana  na maradhi ya saratani ya kongosho.

Gazeti linasema  mwigizaji huyo atakumbukwa  kwa umahiri  wake katika kucheza dansa.

Gazeti  linakumbusha juu ya filamu  inayoitwa dirty  dancing  ya Patrick Swayze  ambayo kila mtu alitaka kuiona mwaka  1989.

Mwandishi /Mtullya-Deutsche Zeitung.

Mhariri/Othman,Miraj