1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maoni ya wahariri,Assad kung'atuka?

Abdu Said Mtullya23 Agosti 2012

Wahariri wanazungumzia juu ya uwezekano wa Rais Assad kung'atuka, uchaguzi nchini Marekani, na kuhusu kupanda kwa bei ya nafaka duniani.

https://p.dw.com/p/15vSQ
Rais Bashar al-Assad wa Syria
Rais Bashar al-Assad wa SyriaPicha: picture-alliance/dpa

Makamu wa Waziri Mkuu wa Syria, Kadri Djamil, alisema mjini Moscow kwamba  suala la Rais  Assad kung'atuka linaweza kujadiliwa. Katika maoni yake juu ya suala  hilo, Mhariri wa gazeti la  "Der Tagesspiegel" anatilia  maanani kwamba , huenda  huo ukawa mwanzo wa kutokea mabadiliko ya kweli nchini  Syria. Mhariri huyo anasema "Ishara inaonekena dhahiri.  Upo wakati na mahala pa kutokea hayo. Kwani Makamu  wa Waziri Mkuu wa  Syria, Djalili, ameshaenda Moscow mara mbili  mnamo  kipindi kifupi cha  wiki mbili. Ndiyo kusema kauli  yake  inapaswa kuzingatiwa kwa makini. Kilichobakia sasa ni kwa  Rais  Putin  kumwalika Rais Bashar al- Assad na kumwambia abakie  Urusi."

Gazeti la "Stuttgarter Zeitung" linazungumzia juu ya kupanda kwa bei ya nafaka duniani. Lakini linahoji kwamba mchakato huo hautokani tu na utengenezaji wa nishati kwa kutumia mimea  na linaeleza kwamba "bei ya nafaka inapanda pia kwa   sababu kiasi kikubwa kinatumika ili kuziba upungufu wa nyama. Na walanguzi nao wanachangia kwa kusababisha ugeugeu wa bei. Lakini yapasa  kusema kwamba ni lazima nishati ya bio itengenezwe kwa manufaa ya kuyalinda mazingira. Ni wazi  kwamba mkabala baina ya chakula na nishati utashtadi, ikiwa hayatafanyika marekebisho, na ikiwa mipaka itavukwa katika uzalishaji  wa nishati kwa kutumia mazao ya kilimo." Na mhariri wa gazeti la "Kolner Stadt-Anzeiger" anaongezea kwa kusema kwamba bado upo wigo wa kuwezesha kuamua juu ya suala la nishati ya bio.  Mhariri  huyo  anaeleza kuwa "viongozi wanaweza kuamua kati ya kutumia mimea ili kuzalisha nishati au kuchanganya na uzalisahi wa nishati kutokana na malighafi..." Na ikiwa itakuwa hivyo, hayatatokea maafa. Lakini mambo hayawezi kuwa hivyo kutokana na mgogoro wa nishati duniani. Na kwa hivyo itawezekana kukidhi mahitaji ya chakula duniani asaa ugavi, utakuwa wa haki.

 Homa ya uchaguzi wa Rais inazidi  kupanda nchini Marekani, kama jinsi inavyoshuhudiwa katika kauli za wanasiasa fulani. Gazeti la "Emder" linaizingatia kauli ya mwanasiasa wa chama cha Republican, Todd Akin, juu ya suala la ubakaji. Linasema: "Mwanasiasa huyo ameyasema kwa sauti kubwa yale yanayofikiriwa na watu wengi wa chama chake cha Republican." Lakini mhariri wa "Badische Neueste Nachrichten" anasema kauli ya mwanasiasa huyo wa chama cha Republican ni sawa na kujifunga goli.  Todd amesema miili ya wanawake ina uwezo asilia wa kujihami dhidi ya ujazito wakati wa alichokiita ubakaji  halali".

Mwandishi:Mtullya abdu/Deustche Zeitungen:

Mhariri: Miraji Othman