1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mapigano yashika kasi Syria

25 Julai 2012

Wanaharakati wa upinzani nchini Syria wanasema mapigano yameshika kasi nchini humo katika maeneo kadha ya mji wa Aleppo, na kufikisha siku ya tano sasa tangu mzozo huo kuingia katika mji huo mkubwa nchini Syria.

https://p.dw.com/p/15eMu
Source News Feed: EMEA Picture Service ,Germany Picture Service A Free Syrian Army soldier waves Syrian opposition flag at the Bab Al-Salam border crossing to Turkey July 22, 2012. Syrian forces regained control of one of two border crossings seized by rebels on the frontier with Iraq, Iraqi officials said, but rebels said they had captured a third border crossing with Turkey, Bab al-Salam north of Aleppo. "Seizing the border crossings does not have strategic importance but it has a psychological impact because it demoralises Assad's force," a senior Syrian army defector in Turkey, Staff Brigadier Faiz Amr, told Reuters by phone. REUTERS/Umit Bektas (SYRIA - Tags: POLITICS)
Kivuko cha mpakani kati ya Syria na UturukiPicha: Reuters

Helikopta za kijeshi zilishambulia leo wilaya ya al-Hajar al-Aswad mjini Damascus.

Kundi linaloangalia haki za binadamu nchini Syria limesema kuwa majeshi ya utawala wa rais Bashar al-Assad pia yametumia makombora katika mashambulio yake dhidi ya wilaya iliyoko upande wa kusini mwa mji huo mkuu.

Mji wa Aleppo katika mapigano

Majeshi ya Syria yamepelekwa kwa wingi katika mji wa Aleppo leo, ambako mashambulizi ya helikopta yamekuwa yakifanyika kuyashambulia maeneo ya waasi, na kuongeza kasi ya mashambulizi dhidi ya mji huo mkubwa kabisa nchini humo, ili kukandamiza uasi dhidi ya rais Bashar al-Assad.

In this image made from amateur video released by the Ugarit News and accessed Monday, July 23, 2012, a Syrian military tank catches on fire during clashes with Syrian government troops in Aleppo, Syria. The Syrian regime acknowledged for the first time Monday that it possessed stockpiles of chemical and biological weapons and said it will only use them in case of a foreign attack and never internally against its own citizens. Aleppo, Syria's biggest city with about 3 million residents, has been the focus of rebel assaults by a newly formed alliance of opposition forces called the Brigade of Unification. (Foto:Ugarit News via AP video/AP/dapd) TV OUT, THE ASSOCIATED PRESS CANNOT INDEPENDENTLY VERIFY THE CONTENT, DATE, LOCATION OR AUTHENTICITY OF THIS MATERIAL
Mapigano katika mji wa AleppoPicha: AP

Uasi nchini Syria ambao umechukua sasa miezi 16, umebadilika kutoka upinzani mdogo katika majimbo ya ndani ya nchi hiyo na kuwa mapambano makali ya udhibiti wa miji miwili muhimu, ya Aleppo na mji mkuu Damascus, ambako mapigano yalizuka wiki iliyopita.

Majeshi ya Syria yameshambulia kwa mizinga eneo la al-Tel mapema leo katika juhudi za kukamata maeneo yanayodhibitiwa na waasi, na kusababisha mtafaruku na kuwalazimisha mamia ya familia kukimbia kutoka eneo hilo, wakaazi na wanaharakati wa upinzani wamesema.

Mmoja wa watu walioshuhudia amesema:

"Hali baada ya mashambulizi hayo , ambapo maafisa wameuwawa ilikuwa hakuna chochote, hakuna mikate, hakuna maji ama umeme, hata katikati ya mji mkuu wa Damascus".

Vivuko vyadhibitiwa na waasi

Wapiganaji wa waasi ambao hawana uongozi wa kati, wamekamata karibu vituo viwili vya vivuko kuingia nchini Uturuki. Magari kadha kutoka Uturuki yameshambuliwa na kuporwa na watu wenye silaha wiki iliyopita katika kivuko cha Bab al-Hawa. Uturuki inatarajia kufunga mpaka wake na Syria baada ya wapiganaji kukamata maeneo kadha ya mpakani.

epa03314291 Syrian rebels celebrate near Aleppo city, in Syria, 22 July 2012. According to media reports on 22 July, Syrian helicopter gunships on 22 July bombarded a rebellious area in the capital Damascus, said the opposition, hours before a meeting of the Arab League foreign ministers on the 17-month conflict. Reports also saying that clashes occured between Syrian rebels and Syrian army in Aleppo. EPA/ABDURRARHMAN AL SHERIF/ANADOLU A TURKEY OUT HANDOUT EDITORIAL USE ONLY/NO SALES/NO ARCHIVES +++(c) dpa - Bildfunk+++
Waasi karibu na mji wa AleppoPicha: picture-alliance/dpa

Wakati huo huo, waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani, Hillary Clinton, amesema kuwa kuna harakati nje ya baraza la usalama la umoja wa mataifa kuunga mkono upinzani.

Washirika kutoa tamko la kuwaunga mkono waasi

"Tunafanya kazi nje ya baraza la usalama la umoja wa mataifa kutuma ujumbe wa wazi wa kuunga mkono upinzani. Kama nilivosema hapo kabla, tunatoa msaada ambao si wa mapigano. Tuna kila sababu ya kuamini kuwa hii itakuwa muhimu kwa upande wa mawasiliano, kimsingi, lakini pia msaada wa matibabu.

U.S. Secretary of State Hillary Clinton talks during a presser with Egyptian foreign minister Ahmed Aboul Gheit, not pictured, following her meeting with President Hosni Mubarak at the Presidential palace in Cairo, Egypt, Wednesday, Nov. 4, 2009. Talks come within the framework of efforts aimed at reviving the Middle East peace process. (AP Photo/Amr Nabil)
Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Hillary ClintonPicha: AP

Silaha za sumu ziko salama

Urusi, wakati huo huo, imesema kuwa imepokea uhakikisho kutoka serikali ya Syria kuwa hazina ya silaha za kemikali iko katika usalama wa hali ya juu. Hayo yamesemwa na naibu waziri wa mambo ya kigeni wa Urusi, Gennady Gatilov, wakati akizungumza na shirika la habari la nchi hiyo, Itar-Tass.

Pia Urusi imeshutumu leo duru nyingine ya vikwazo vya Umoja wa Ulaya dhidi ya Syria.

Nae balozi wa Syria nchini Cyprus, Lamia al-Hariri, ameacha madaraka yake na kukimbilia nchini Qatar.

Mwandishi : Sekione Kitojo / rtre/ape/dpae

Mhariri : Othman Miraji