1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

"Mapigano yasitishwe Congo"

21 Novemba 2012

Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio kuhusu Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, baada ya waasi wa M23 kuuteka mji wa Goma Jumanne . Azimio hilo limetoa wito wa kusitishwa mapigano mara moja.

https://p.dw.com/p/16n9z
The United Nations Security Council meets at the United Nations in New York to discuss the ongoing violence in Syria April 21, 2012. The U.N. Security Council unanimously adopted a resolution on Saturday that authorizes an initial deployment of up to 300 unarmed military observers to Syria for three months to monitor a fragile week-old ceasefire in a 13-month old conflict. REUTERS/Allison Joyce (UNITED STATES - Tags: POLITICS)
Baraza la Usalama la Umoja wa MataifaPicha: Reuters

Kwa mujibu wa maelezo ya mwandishi wa Dw aliyekuwepo mjini New York baraza hilo limepanga kuwawekea vikwazo viongozi wa kundi hilo la M23 sambamba wanaowasaidia kutoka nje ya DRC. Hata hivyo hawakufafanmua zaidi kuhusu wasaidizi hao.

Aidha baraza hilo limemuomba katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon atoe mapendekezo yake kwa baraza hilo ya namna ya kufanikisha kumalizika kwa mzozo katika eneo la Kivu.

Nguvu za kijeshi ziongezwe

Sambamba na hilo limesema kuna umuhimu wa kukiongezea nguvu zaidi kikosi cha umoja wa mataifa nchini humo MONUSCO ili kiweze kujihami pamoja na kuwalinda raia.

A MONUSCO (the UN mission in Democratic Republic of Congo) soldier patrols in the deserted streets of Goma late on October 16, 2012. Amnesty International last week called on the Democratic Republic of Congo to put an end to the fighting in the east of the country where several local and foreign armed groups are committing abuses. AFP PHOTO / JUNIOR D. KANNAH (Photo credit should read JUNIOR D.KANNAH/AFP/Getty Images)
Kikosi cha usalama cha Umoja wa MataifaPicha: D.KANNAH/AFP/Getty Images

Pamoja na mambo mengine katika mapendekezo yake kwa baraza la usalama serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo ilitaka kuwepo kwa aufafanuzi zaidi kuhusi kwa rwanda katika machafuko hayo ya mashariki mwa Congo.

Rwanda yaendelea kujitetetea

Kwa mujibu wa afisa mwandamzi wa Rwanda katika umoja wa Mataifa, Olivier Nduguhungirehe aliendelea kukana kuhusika kwa taifa lake na kundi la waasi wa M23. Hata hivyo afisa huyoamesema kiniachoweza kumaliza machafuko hayo ni mazungumzo kati ya waasi na serikali ya Congo.

People flee as fighting erupts between the M23 rebels and Congolese army near the airport at Goma, Congo, Monday, Nov. 19, 2012. Rebels believed to be backed by Rwanda fired mortars and machine guns Monday in a village on the outskirts of the provincial capital of Goma and threatened to attack the city which is protected by ragtag Congolese government troops backed by United Nations peacekeepers. The gunfire and explosions erupted in the early afternoon, hours after the M23 rebels said they were halting fighting in order to negotiate with the government of Congo. (Foto:Melanie Gouby/AP/dapd).
Wakimbizi kutoka GomaPicha: AP

Katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo kwenyewe hali mjini Goma inaelezwa kuwa mbaya zaidi huku idadi kubwa ya wananchi wakiwa katika hofu ya usalama wao, wafungwa waliyoko magerezani wamefunguliwa. Kupata zaidi juu ya kile kinachoendelea, Sudi Mnette amezungumza na Mratibu wa Jumuiya ya Kiraia, Mustafa Mwiti akiwa Goma. Kusikiliza mahojiano hayo bonyeza kitufe cha alama ya kusikiliza masikioni hapo nchini.

Mwandishi:Amina Abubkar
Mhariri:Mohammed Abdul-Rahman