1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mauwaji ya Waasi kaskazini ya Mali

14 Februari 2012

Jumuia ya kimataifa imelaani vikali mauwaji ya kinyama yaliyofanywa na waasi wa Touareg kaskazini mwa jamhuri ya Mali.Mapigano katika eneo hilo yamepelekea maelfu ya watu kuyapa kisogo maskani yao.

https://p.dw.com/p/142zi
Manöver des malischen Militärs gegen den islamistischen Terrorismus im Sahel; die malische Armee wird dabei von westlichen Militärexperten beraten
Luteka za jeshi la MaliPicha: picture-alliance/Désirée von Trotha

Wanajeshi kadhaa wa serikali na raia wa kawaida wameuliwa huko Aguelhok,kaskazini mashariki ya jamahuri ya Mali tangu waasi wa Touareg walipoanza hujuma zao kati kati ya mwezi uliopita.

Ripoti ya waziri wa ushirikiano wa Ufaransa,Henri de Raincourt kuhusu mauwaji hayo,imethibitishwa na jeshi la Mali mjini Bamako.

"Mauwaji ya kinyama yamefanyika huko Aguelhok,wanajeshi,raia wa kawaida,inasemekana watu wasiopungua mia moja,walitekwa nyara na baadae kuuliwa kikatili kabisa" amesema waziri waziri huyo wa ushirikiano wa Ufaransa.

Henri der Raincourt aliyeitembelea Mali february tisa iliyopita hakutaja nani walikuwa nyuma ya mashambulio hayo,alisema tu mtindo wa mauwaji hayo unalingana na ule unaotumiwa na Al Qaida."

Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Ufaransa,Alain Juppé, nae pia amelaani mauwaji hayo akisema lakini"haijulikani bado nafasi iliyoshikiliwa na Al Qaida au Aqmi katika mashambulio hayo.

In this May 17, 2010 file photo, a nomad from the Tuareg tribe of the Sahara Desert brings his herd for vaccination to a team of U.S. Special Forces in the Sahara Desert handing out aid near the town of Gao in northeastern Mali. With almost no resistance, al-Qaida in the Islamic Maghreb, or AQIM, is implanting itself in Africa's soft tissue, choosing as its host Mali, one of the poorest nations on earth. Although AQIM's leaders are Algerian, it recruits people from Mali, including 60 to 80 Tuareg fighters, the olive-skinned nomads who live in the Sahara desert, according to a security expert who spoke anonymously because of the sensitivity of the matter. (AP Photo/Alfred de Montesquiou, File)
Wahamiaji wa TouaregPicha: AP

Mkuu wa idara ya upelelezi na uhusiano wa jamii nchini Mali,kanali Idrissa Traoré amethibitisaha mauwaji ya kinyama yaliyofanyika january 24 huko Aquelhok na kuongeza;raia pia wameuliwa.

"Mauwaji ya kikatili yametokea siku hiyo,watu wamekatwa vichwa,wengine wamepigwa risasi kichwani,kulikuwa na hata raia miongoni mwa wahanga wa mauwaji hayo ambayo hayawezi kufanywa na yeyote mwengine isipokuwa wafuasi wa Al Qaida katika eneo la maghreb-Aqmi" amesema mkuu huyo wa idara ya upelelezi ya Mali.

Hakutaja idadi halisi ya wahanga lakini afisa mmoja wa jeshi aliyeshiriki kuwazika wahanga hao amesema wanajeshi 97 wameuliwa.

January 26 iliyopita serikali ya Mali ilisema wafuasi wa Aqmi na waasi wa Touareg washambulia kwa pamoja mji wa Aguelhok.

Aguelhok,mji ulioko kilomita 150 kaskazini mashariki ya Kidal umegeuka kuwa kitovu cha mapigano yaliyopelekea watu wasiopungua elfu nne kuyapa kisogo maskani yao.

Tume ya shirika la kimataifa la Msalaba mwekundu na lile la Mali imefika katika maeneo walikokimbilia wakimbizi hao ili kuwahudumia.

Blick auf den Regierungspalast in Malis Hauptstadt Bamako. (undatierte Aufnahme)
Kasri la rais wa Mali mjini BamakoPicha: picture-alliance/dpa

Kuna maelfu waliotawanyika ndani nchini Mali na wengine waliokimbilia Mauritania,Niger na Burkina Faso.

Jana rais Amadou TOumani Toure wa Mali alifanya ziara fupi mjini Ouagadougou na kuzungumza na kiongozi mwenzake wa Burkina Faso Blaise Compaore ambae nchi yake inawapokea wakimbizi elfu kumi wa Mali.Miongoni mwa wakimbizi hao kuna wanajeshi akiwemo mkuu wa vikosi vya gendarmerie aliyetangaza hivi karibuni kudai uhuru wa eneo la kaskazini la Mali.Serikali ya Mali inataka mwanajeshi huyo anyamazishwe au arejeshwe nyumbani.

Mwandishi:Hamidou Oummilkheir/Afp

Mhariri:Yusuf Saumu