1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mfuko wa uokozi wa euro mashakani

Sekione Kitojo17 Januari 2012

Mfuko wa uokozi wa mataifa yenye madeni katika eneo la sarafu ya euro uko katika mbinyo mkali baada ya kupunguziwa hadhi yake ya kuaminika na masoko kutoka A tatu hadi A mbili.

https://p.dw.com/p/13kgs
The offices (R) of credit firm Fitch Ratings are pictured in London, Britain 29 April 2010. Fitch Ratings is one of the major rating agencies that sort good investments from junk. Other rating agencies include Standard & Poor's, and Moody's Corp. Standard & Poor's cut Greece sovereign debt to 'junk' status 27 April and dropped Portugal's down two notches in a downgrade that sent financial markets from London to Hong Kong plunging. EPA/ANDY RAIN +++(c) dpa - Bildfunk+++
Ofisi za mjini London za shirika la kuweka viwango la FitchPicha: picture-alliance/dpa

Mfuko wa uokozi hauaminiki

Mashirika mengine makubwa ya upangaji viwango , Moody's and Fitch tathmini yao kwa mfuko wa uokozi wa mataifa ya umoja wa sarafu ya euro wenye thamani ya euro bilioni 440 bado ipo katika alama A tatu. Standard and Poor's kinyume chake imepunguza A moja na kuupa mfuko huo wa EFSF A mbili, kwasababu shirika hilo linaziona Ufaransa na Austria , nchi ambazo zinachangia kwa kiasi kikubwa katika mfuko huo, haziaminiki tena kuwa na uwezo wa kukopa katika masoko ya kimataifa.

Mahesabu ni rahisi kabisa , wakati sehemu ya wachangiaji , ambazo ni nchi za umoja wa safaru ya euro zinapungukiwa na uwezo wa kuaminika kukopa, na mfuko huo pia unapoteza uwezo huo. Pamoja na hayo hii haihusiki na kuubana mfuko huo kulipia riba kubwa, ikiwa na maana ya gharama za juu kwa mfuko huo wa EFSF katika kupata michango yake. Kwa hiyo mfuko huo unalitambua hilo.

Waziri wa fedha wa Ujerumani Wolfgang Schäuble ameliweka wazi hilo katika mahojiano na radio ya Ujerumani. Mbunge kutoka chama cha CDU katika bunge la Ujerumani Bundestag Michael Meister amesema kuwa ili kuweza kupata tathmini ya juu kutoka kwa mashirika haya na kubakia na alama za juu , ni lazima mataifa husika yaongeze dhamana kwa ajili ya mfuko huo.

Ujerumani haijashushwa

Ujerumani haikushushwa kiwango chake kwa hiyo haipaswi pia kutoa uhakika wa kupatikana kwa euro bilioni 211. Ufaransa na Austria , zimeshushwa na shirika la Standard and Poor's na kupewa alama ya A mbili badala ya tatu. Nchi hizi amesema Meister kuwa zinapaswa kufanya zaidi.

Kwa mtazamo wa waziri wa fedha wa Ujerumani Schäuble hata hivyo anapingana na mawazo hayo na kwamba uhakika wa mfuko huo kuweza kulipa fedha katika muda wa miezi ijayo upo bila shaka.

Berlin/ ARCHIV: Bundesfinanzminister Wolfgang Schaeuble (CDU) gestikuliert waehrend eines Interviews in der Zentrale der Nachrichtenagentur dapd in Berlin (Foto vom 08.12.11) . Schaeuble lehnt die Forderung des Vorstandsvorsitzenden der Deutschen Bank Josef Ackermann nach einer Beteiligung der oeffentlichen Glaeubiger an der Umschuldung Griechenlands ab. "Der oeffentliche Sektor traegt ja sowieso das, was der Privatsektor nicht uebernimmt", sagte der Finanzminister dem "Handelsblatt" (Freitagausgabe vom 30.12.11). "Insofern muss sich niemand bei den privaten Finanzinstituten Gedanken machen, dass sich der oeffentliche Sektor nicht genuegend in Griechenland engagiert." Foto: Clemens Bilan/dapd
Waziri wa fedha wa Ujerumani Wolfgang SchäublePicha: dapd

Hivi sasa imebakia tu Ujerumani kuwa katika hadhi ya juu pamoja na Uholanzi, Finnland na Luxemburg. Inasubiriwa kwa hamu kuona ni masharti gani mfuko huo wa uokozi utatoa leo Jumanne katika kugharamia masoko ya fedha. Rais wa benki kuu ya umoja wa Ulaya Mario Draghi amesema jana katika bunge la ulaya mjini Strassburg kuwa kushushwa huko kuna gharama yake.

Kushushwa kwa hadhi ya mfuko wa EFSF kuna matokeo yake, ambapo iwapo mfuko huo unataka kubakia na hadhi ya alama ya A tatu , inaweza kukopesha kwa kiwango kidogo, ama iwapo haitaweza kubakia na hadhi hiyo bei na gharama za ukopeshaji zitapanda Ama hatua mbadala ni kwamba , ibaki na kiwango chake hicho hicho, iendelee kukopesha kwa uwezo huo huo, bei iwe ile ile, lakini ipate ,michango. Ni lazima kupata michango ya ziada kutoka kwa mataifa yale yenye alama A tatu.

Sarkozy aionya Ulaya

Kutokana na kushushwa kwa hadhi ya kuaminika kwa mfuko wa uokozi katika mataifa ya sarafu ya euro rais wa ufaransa Nicolas Sarkozy ameonya pia kuwa Ulaya inakabiliwa na mzozo mkubwa, na inapaswa kutafuta njia mpya ya kukuza uchumi wake.

French President Nicolas Sarkozy addresses the 20th congress of the European People's Party, EPP, Thursday, Dec. 8, 2011 in Marseille, southern France. The leaders of France and Germany hoped to rally fellow European conservatives on Thursday around their latest bid to save the euro currency from collapsing under the weight of huge state debt. (Foto:Jean-Paul Pelissier, Pool/AP/dapd)
rais wa Ufaransa Nicolas SarkozyPicha: dapd

Sarkozy ameyasema hayo baada ya mazungumzo yake na waziri mkuu wa Uhispania Rajoy mjini Madrid kuwa sasa mataifa ya ulaya yanapaswa kupunguza matumizi, kupunguza nakisi katika bajeti zao na kutatua matatizo ya ushindani wa ndani.

Mwandishi : Bernd Riegert/ZR/ Sekione Kitojo

Mhariri: Mohammed Khelef

http://www.dw-world.de/dw/article/0,,15669647,00.html