1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mgogoro serikali ya Uingereza kuelekea Brexit

Iddi Ssessanga
13 Juni 2017

Matokeo mabaya ya chama cha Conservative katika uchaguzi yameiweka pabaya Uingereza kuelekea majadiliano ya Brexit. Wakati May akijaribu kubakia madarakani, viongozi wa EU wamesema mazungumzo ya Brexit hayatarefushwa.

https://p.dw.com/p/2ebFl
Großbritannien Theresa May Gottesdienst in Sonning
Picha: Reuters/N. Hall

Wakati waziri mkuu Theresa May alipozindua kifungu cha 50 cha Mkataba wa Lisbon mwezi Machi, na hivyo kuanzisha mchakato rasmi wa Uingereza kujiondoa katika Umoja wa Ulaya, hakujua kwamba muda si mrefu atakuwa anapigania maisha yake ya kisiasa.

Ibara ya 50 ambayo haikusanifiwa kurahisisha mambo kwa nchi yoyote inayotaka kujitoa kwenye Umoja wa Ulaya, inaweka muda maalumu wa miaka miwili wa mazungumzo, ikiipa Uingereza hadi Machi 2019 kukamilisha mazungumzo.

Viongozi wa Umoja wa Ulaya wameashiria kuwa hawataki kurefusha muda huo: "Hatujui lini mazungumzo ya Brexit yatakapaonza. Tunajua lini yanapaswa kumalizika," alisema rais wa baraza la Ulaya Donald Tusk kwenye ukurasa wa twitta siku ya Ijumaa.

Arlene Foster, Parteichefin der nordirischen DUP und Theresa May
Waziri Mkuu Theresa May akiwa na kiongozi wa chama cha Democratic Unionist Arlene Foster, ambacho anataka kushirikiana nacho kuimarisha serikali yake.Picha: picture-alliance/empics/C. McQuillan

Hatari ya mchakato kuvurugika zaidi

Mazungumzo yalitarajiwa kuanza Juni 19, lakini matokeo ya kushitukiza ya uchaguzi Juni 9 ambamo Wahafidhina walipoteza wingi wao bungeni, hilo linazidi kutowezekana. "Hakuna shaka kabisaa kwamba Uingereza inaingia katika majadiliano hayo ikiwa dhaifu, na kukosekana kwa mamlaka ya wazi kunahatarisha kuvuruga zaidi mchakato ambao tayari ulionekana kuwa mgumu," amesema Sophie Gaston, mkuu wa miradi ya kimataifa kutosha shirika la ushauri la Demos.

Amesema hatua ya May kuzindua ibara ya 50 kabla ya uchaguzi ilikuwa ya kiburi na imeiacha nchi hiyo ikiwa katika nafasi dhaifu kabisaa. Amesema inawezekana wakachelewesha kuanza kwa majadiliano kadiri wapendavyo, lakini muda hautasimama kwenye tarehe yake ya mwisho.

May anataka kubuni muungano na chama cha Democratic Union cha Ireland ya Kaskazini DUP, ambacho kitawaimarisha Wahafadhina katika serikali ya wingi mdogo, lakini ambayo bado haina uhakika. Wakati majadiliano na DUP yakiendelea, May amekamilisha muundo wa baraza lake la mawaziri.

Njia ya mashaka

Bado haijajulikana ni athari zipi nafasi hii iliopungua ya chama cha Conservative itakuwa nazo kuhusu mazungumzo ya Brexit. Baadhi ya wadadisi wameyafasri matokeo ya uchaguzi kama kukataliwa kwa mkakati wa May mpaka sasa - lakini ni taswira mchanaganyiko.

UK | Britische Presse nach Neuwahl in Großbritannien
Mpigapicha wa TV akisoma gazeti la Daily Mirror likiwa na kichwa cha "Muungano wa wapumbavu", siku moja baada ya uchaguzi mkuu kutoa bunge lisilo na mshisndi wa wazi na waziri mkuu Theresa May kuunda serikali ya wingi mdogo.Picha: Getty Images/AFP/J. Tallis

Licha ya ukubwa wa changamoto ya kikatiba inayoikabili Uingereza, ushirikiano kati ya vyama hauonekani kuwa kwenye agenda, mnamo wakati uahasama wa kivyama unazidi kuongezeka. Gaston anasema lingekuwa jambo la manufaa kwa taifa kuwa na vichwa bora vikishirikiana - lakini mashaka na fursa yanavyotoa matokeo hayo ya vurugu kwa Conservatives na Labour vinamaanisha kuwa kutakuwa na ari kubwa ya kivyama kutoka pande zote mbili.

Wakati May akipambana kubakia madarakani, maswali yameanza kuulizwa kuhusu uwezo wake wa kuongoza Uingereza kupita katika kipindi hiki. Mwanasheria ambaye pia ni mtangazi David Allen Green, aliiambia DW kuwa hasara itakayosabishwa na Brexit itasababishwa zaidi moja kwa moja na mfululizo wa maamuzi mabaya ya May kuliko matokeo halisi ya kura ya maoni.

Anasema wakati Uingereza ikiwa katika mwezi wa tatu wa mchakato wa Ibara ya 50, inaonekana taifa hilo liko katika nafasi mbaya zaidi kutokana masihara ya May ya uchaguzi mkuu kuliko wakati Uingereza ilipotoa taarifa hiyo.

Mwandishi: Samira Shackle, DW

Ripoti: Iddi Ssessanga

Mhariri:Caro Robi