1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Misaada yaanza kuwasili Ufilipino

15 Novemba 2013

Idadi ya watu waliofariki Ufilipino kutokana na kimbunga Haiyan imeongezeka mara dufu, na kufikia 4,000, wakati helikopta za jeshi la Marekani na meli zimeanza kupeleka misaada na madaktari katika eneo la maafa.

https://p.dw.com/p/1AI9D
TACLOBAN, PHILLIPINES - NOVEMBER 14: In this handout provided by the U.S. Navy, hospital Corpsman 3rd Class Eric Chiarito (L) of Hyde Park, N.Y., and Marine Sgt. Jonathan Thornton, of Lake Havasu, Arizonia, load supplies onto a forklift at Tacloban Air Base in support of Operation Damayan November 14, 2013 in Tacloban, the Phillipines. The George Washington Carrier Strike Group and the 3rd Marine Expeditionary Brigade are assisting the Philippine government in response to the aftermath of Typhoon Haiyan (Yolanda). (Photo by Ricardo R. Guzman/U.S. Navy via Getty Images)
Misaada ya kimataifa inayopelekwa TaclobanPicha: Getty Images

Katika mji wa Merida uliopo kisiwani Leyte , taka bado zimezagaa barabarani kutokana na mabaki ya majengo yaliyoporomoka.

Kimbunga Haiyan kimeshambulia mno katika eneo hilo. Takriban wiki moja baada ya kimbunga hicho wakaazi wa mji wa Merida wameanza kazi ya ujenzi mpya na baadhi ya nyumba zimeanza kutumika. Mvua bado inaendelea kunyesha na wakaazi wa mji huo hujikusanya pamoja katika nyumba ambazo zimebakia na paa juu yake na zile ambazo zimeanza kujengwa na wanajihifadhi kwa pamoja.

Juhudi za kuwasaidia watu walionusurika na kimbunga Haiyan nchini Ufilipino zimeongezeka kuanzia leo, licha ya kuwa serikali imekiri kuwa kasi yale bado ni ndogo.

TACLOBAN, PHILIPPINES - NOVEMBER 14: US Bell Boeing V-22 Osprey arrive at the airport to transport humanitarian workers to typhoon affected areas on November 14, 2013 in Tacloban, Leyte, Philippines to help people affected by typhoon. Typhoon Haiyan which ripped through Philippines over the weekend has been described as one of the most powerful typhoons ever to hit land, leaving thousands dead and hundreds of thousands homeless. Countries all over the world have pledged relief aid to help support those affected by the typhoon, however damage to the airport and roads have made moving the aid into the most affected areas very difficult. With dead bodies left out in the open air and very limited food, water and shelter, health concerns are growing. (Photo by Jeoffrey Maitem/Getty Images)
Helikopta za jeshi la Marekani zikipeleka misaada UfilipinoPicha: Getty Images

Waziri wa mambo ya ndani Mar Roxas amesema kuwa katika mji wa Tacloban , mji mkuu wa jimbo lililoathirika kwa kiasi kikubwa la Leyte, malori yaliyobeba mahitaji mbali mbali yamefika katika miji 30 kati ya 40 katika jimbo hilo.

Usafishaji waanza

Wafanyakazi wakiwa na misumeno ya umeme wamekuwa wakikata miti iliyoanguka mjini Tacloban wakati malori yakibeba miili ya watu waliofariki pamoja na taka zilizozagaa mitaani, na wengine wakikarabati nyumba zilizoporomoka.

Rais Benigno Aquino, ameshindwa kutambua ukubwa wa maafa hayo, na amekosolewa kutokana na kasi ndogo ya usambazaji wa misaada pamoja na makadirio yenye utata ya watu waliofariki, hususan katika mji wa Tacloban, mji ambao umeathirika mno na kimbunga hicho.

epa03943724 A picture made available by the Malacanang Photo Bureau shows President Benigno S. Aquino III (2-L) gives out water to families displaced by Typhoon Haiyan during his visit to Tacloban City in the province of Leyte in Philippines, 10 November 2013. Typhoon Haiyan tore through the eastern and central Philippines beginning 08 November, flattening homes, toppling power lines and knocking out communications. Fierce winds ripped roofs off buildings as raging floodwaters swept debris and left vehicles piled on top of each other on the battered streets. The official death toll was 138, according to the national disaster relief agency. But official said, the toll could reach 10,000 in one city alone. EPA/RYAN LIM/ MALACANANG PHOTO BUREAU HANDOUT EDITORIAL USE ONLY/NO SALES
Rais wa Ufilipino Benigno S. Aquino akiwafariji wahanga wa maafa ya kimbunga HaiyanPicha: picture-alliance/dpa

Meya aomba radhi

Taarifa katika jengo la halmashauri ya mji wa Tacloban imekadiria kuwa watu 4,000 wamefariki , ikiwa ni ongezeko kutoka idadi ya watu 2,000 waliotangazwa siku moja kabla katika mji huo pekee. Hata hivyo meya wa Tacloban Alfred Romualdez aliomba radhi na kusema kuwa idadi hiyo ni kwa eneo lote la kati la Ufilipino.

Waziri wa mambo ya ndani Mar Roxas amesema kuwa juhudi za kutoa misaada zinaendelea, licha ya kuwa kasi yake ni ndogo bado. Amesema kuwa kila siku inakuwa bora zaidi kuliko siku iliyopita. Haiwezekani kasi kuwa kubwa katika hali kama hii kwasababu watu wengi mno wameathirika na miundo mbinu imeharibika.

Sandra Bulling kutoka katika shirika la kutoa misaada la Care International amesema misaada imeanza kuwafikia walengwa.

"Kwa hivi sasa misaada yetu ya chakula imo njiani kutoka Manila kuja hapa kisiwani. Misaada hiyo itawasili kesho na tutaweza haraka iwezekanavyo kugawa misaada katika eneo la Mormoc. Na mpango ni kwamba katika muda wa siku chache zijazo tutaweza kutumia fursa hii, kufikisha misaada hiyo Merida ama Isabel. Na katika siku chache zijazo tutaleta vifaa vya ujenzi, ili watu waweze kupata mahali pa kuishi."

People wait behind a fence at the Tacloban airport for an airlift to Manila in the aftermath of super typhoon Haiyan, in Tacloban November 14, 2013. Thousands of people who were affected by typhoon Haiyan lined up at the army checkpoint near the Tacloban airport tower on Thursday wait to be airlifted to Manila on C-130 planes provided by the U.S. Marines and the U.S. Air Force. REUTERS/Wolfgang Rattay (PHILIPPINES - Tags: DISASTER ENVIRONMENT)
Bado mvua inanyesha na hakuna mahali pa kujihifadhiPicha: Reuters

Lakini wakati juhudi za kutoa misaada zikiendelea , wataalamu kutoka shirika la afya ulimwenguni WHO pamoja na mashirika mengine yamerudia ushauri wao kuwa serikali ya Ufilipino inapaswa kulenga juhudi zake za kutoa misaada kwa watu walionusurika, badala ya kushughulikia waliofariki.

Mwandishi: Peter Hille / ZR / Sekione Kitojo

Mhariri: Daniel Gakuba