Mji wa Pyeongchang kuwa mwenyeji wa michezo ya Olympics 2018
7 Julai 2011Matangazo
Mji wa Pyeongchang, umeshinda zabuni kwa kauli mbiu ya "upeo wa fikra mpya'', baada ya kupata ushindi wa kura nyingi dhidi ya miji mingine iliyokuwa ikiigombea nafasi hiyo, Munich wa Ujerumani na mji wa Annecy wa Ufaransa, kutoka katika kamati ya Kimataifa ya Olympic.
Awali akizungumzia ushindi huo wa Korea kusini, Rais wa kamati ya Kimataifa ya Olympic Jacques Rogge amesema ushindi huo mkubwa uliopata mji wa Pyeongchang, katika awamu ya kwanza ya uchaguzi, umemshangaza hata yeye binafsi.