1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MOGADISHU: Kituo cha polisi kimevamiwa Somalia

3 Agosti 2007
https://p.dw.com/p/CBck

Si chini ya watu 10 wameuawa katika mashambulizi yaliyozuka mji mkuu wa Somalia,Mogadishu ikishukiwa kuwa yamefanywa na waasi wa makundi ya Kiislamu.Katika shambulio moja peke yake,watu wasiopungua 9 waliuaw,baada ya kituo cha polisi kuvamiwa wakati wa usiku,kaskazini mwa Mogadishu. Mpita njia mmoja pia aliuawa,baada ya mshambulizi kurusha gruneti kwenye mkahawa unaotumiwa sana na maafisa wa kijeshi,kusini mwa Mogadishu.