1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MOGADISHU: Majeshi ya Ethiopia yaanza kuondoka Somalia

23 Januari 2007
https://p.dw.com/p/CCYh

Majeshi ya Ethiopia yameanza leo kuondoka mjini Mogadishu Somalia, wiki nne baada ya kuwasaidia wanajeshi wa serikali ya mpito ya Somalia kuwafurusha wanamamgambo wa mahakama za kiislamu kutoka mjini humo.

Waziri wa mambo ya ndani wa serikali ya mpito ya Somalia, Hussein Mohammed Farah Aideed, amesema kikosi cha Umoja wa Afrika kitachukua mahala pa jeshi la Ethiopia katika juma moja lijalo. Hakuna uhakika lakini ikiwa wanajeshi wa Umoja wa Afrika wataweza kuidhibiti hali ndani ya Somalia.