1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MOGADISHU: Mripuko umeua watu 4 nchini Somalia

11 Februari 2007
https://p.dw.com/p/CCT9

Mripuko uliotokea wakati wa sherehe za kijeshi katika mji wa bandari wa Kismayu nchini Somalia, umeua watu 4 na wengine zaidi ya 20 wamejeruhiwa. Mashahidi wamesema,maafisa wa kijeshi wa ngazi ya juu na wajumbe wa polisi ni miongoni mwa wale waliojeruhiwa.Tangu vikosi vya serikali ya Somalia kuwatimua wanamgambo wa Kiislamu kwa msaada wa majeshi ya Ethiopia,Somalia inashuhudia mashambulio takriban kila siku.Serikali ya Somalia inaulaumu Muungano wa Kiislamu kuhusika na mashambulio hayo.Muungano huo ulidhibiti eneo la kusini mwa nchi kwa muda wa miezi sita kabla ya kutimuliwa majuma machache yaliopita.