MOGADISHU: Polisi ameuawa katika shambulio la waasi
19 Juni 2007Matangazo
Polisi mmoja ameuawa na watu waliobeba silaha katika wimbi la mashambulio yanayofanywa dhidi ya vituo vya serikali katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.Polisi wengine 3 pia walijeruhiwa katika shambulizi hilo.Kwa mujibu wa afisa wa polisi,waasi waliokuwa na silaha kubwa walishambulia kituo cha polisi wakati wa usiku katika mtaa wa Huriwa,kaskazini mwa Mogadishu.