1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MOGADISHU:Al Qaida yateua kamanda huko Somalia

22 Machi 2007
https://p.dw.com/p/CCGU

Serikali ya mpito ya Somalia imesema kuwa kundi la Al Qaida, limemteua kamanda kijana wa wapiganaji wa kiislam kuwa kiongozi wake katika nchi hiyo ya pembe ya afrika.

Waziri wa Ulinzi wa serikali hiyo Jalal Ali Jelle amesema kuwa, kijana huyo, Aden Hashi Ayro mwenye umri wa miaka 30 na mzaliwa wa Afghanistan ni komandoo aliyefuzu.

Amesema kuwa Aden ni kiongozi wa kundi linaloagopwa la Shabab na amekuwa akihusika na kuongezeka kwa mapigano.

Kauli hiyo ya waziri wa ulinzi wa Somalia inakuja mnamo wakati nchi hiyo imeingia katika siku ya pili ya mapigano makali mjini Mogadishu.

Marekani na Somalia kwa muda mrefu zimekuwa zikimlaumu Hashi Ayro na viongozi wengine wa mahakama za kiislam kuhusika na mtandao wa Al Qaida