1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MOSCOW: Gorbachev apendekeza Kohl apewe Tuzo ya Amani

12 Juni 2007
https://p.dw.com/p/CBsP

Mikhail Gorbachev aliekuwa rais wa Soviet Union ya zamani,amependekeza Kansela wa zamani wa Ujerumani,Helmut Kohl apewe Tuzo ya Amani ya Nobel.Gorbachev alieanzisha mfumo wa demokrasia nchini mwake katika miaka ya 80 ameandika barua kwa kamati ya Nobel mjini Oslo.Amesema,Kohl alichukua nafasi muhimu katika matokeo ya kihistoria yaliyokwenda kwa amani.Gorbachev binafsi alipewa Tuzo ya Amani ya Nobel mwaka 1990.