1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MOSCOW: Ndege ya shehena yanguka nchini Urusi

29 Julai 2007
https://p.dw.com/p/CBeC

Ndege ya shehena aina ya Antonov,imeanguka muda mfupi tu baada ya kuondoka kwenye uwanja wa ndege wa Domodedovo mjini Moscow.Maafisa wamesema,watu wote 8 waliokuwemo ndani ya ndege hiyo wamefariki.Sababu ya ajali kwa hivi sasa,bado haijulikani.Ajali hiyo imetokea saa chache tu baada ya helikopta moja kuanguka katika eneo la Udmurtiya kwenye milima ya Ural ya Urusi.Kwa mujibu wa maafisa,helikopta hiyo iligusa kebu za umeme kabla ya kuanguka kwenye bwawa.